Monday, November 25

SAKATA LA UBAKAJI LAENDELEA, PROFESA JUMA KAPUYA ABURUZWA POLISI KWA TUHUMA ZA KUBAKA.

HATIMAYE binti anayedaiwa kubakwa na Mbunge wa Urambo Magharibi, Profesa Juma Kapuya (CCM), amefungua jalada Polisi dhidi ya mbunge huyo.

Habari za kipolisi ambazo Tanzania Dama limezipata, zinasema kuwa binti huyo ambaye anadai kubakwa na kisha kutishiwa kuuawa na Profesa Kapuya, amefungua jalada namba OB/RB/21124/13 katika Kituo cha Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

Harakati za kufungua jalada hilo zilianza juzi jioni na kuendelea hadi jana ambapo polisi walitumia zaidi ya saa 12 kumhoji binti huyo anayedaiwa kubakwa ili kupata ukweli wa sakata hilo.

Akiwa kituoni hapo, binti huyo alikutana na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi ya Oysterbay (OCD) na OC-CID wake na kutoa maelezo ya awali kabla ya viongozi hao kumruhusu ayaweke malalamiko yake katika maandishi kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius  Wambura, alikiri polisi kufungua jalada hilo na kuongeza kwamba hivi sasa wanafanya uchunguzi kubaini kama ujumbe ulio katika simu ya binti anayedai kubakwa na kutishiwa maisha unatoka katika simu ya  mbunge huyo.

“Tumefungua jalada, lipo kwa ajili ya uchunguzi na tukibaini kuwa ni nani anahusika na tuhuma hizo tutamsaka na kumkamata popote alipo,” alisema Wambura.

Habari zaidi zinasema polisi wamechukua namba ya Kapuya inayodaiwa kutumika mara kwa mara kutuma ujumbe mfupi wa maneno kwa binti huyo, akitishiwa kuuawa.

Simu hiyo namba 0784993930 inayodaiwa kumilikiwa na Profesa Kapuya, mbali ya kutuma ujumbe mfupi wa maneno ya kutishia kuua, pia ndiyo inayodaiwa kutumika kutuma pesa kwa njia ya mtandao kwenda kwa binti huyo.

Moja ya ujumbe wa vitisho unaodaiwa kutumwa na Kapuya kupitia simu hiyo unasomeka hivi;  “Mkiuawa itakuwa vizuri…itawapunguzia gharama za kuishi, usitake kugombana na serikali mtoto mdogo kama wewe, sisi ndiyo wenye nchi yetu, mwenye hilo gazeti ni Mbowe sasa mwambieni nyumba ya kuishi si mmemuingizia hela leo? Mnatumika tu bure watu wanaingiza hela nyingi, ila mmenitibua lazima niwaue wiki hii haitaisha, nitapiga kambi kote, jana si wamekuficha tuone utalindwa milele maana washatengeneza hela, lazima mvae sanda tu hilo sio ombi ni wajibu wenu, mnajitia na nyie mafia watoto siyo, watoto wetu wanauza unga nani anawakamata? Nani atapingana nasi.”

Pia simu hiyo iliwahi kutuma ujumbe mfupi wa maneno unaosomeka hivi; “Ni lazima nitakuua wewe na ndugu yako na atakaetaka kuwasaidia, huyo Sitta asijiingize kwenu, yaani nitakuua tena sijui leo mtalala wapi? We unadhani nani atakaenifunga, ndo nishakupa ukimwi, sasa nakutaka uache mara moja kuongea na mtu, nitakuwinda popote tuone.”

Mbali na kutishia kumuua binti huyo na ndugu yake na mtu mwingine yeyote atakayejitokeza kumsaidia, Tanzania Daima limenasa baadhi ya mawasilino ya simu za ujumbe mfupi wa kuhamisha fedha kutoka kwa Profesa Kapuya kwenda kwa binti huyo ambaye mbunge huyo alikana kumfahamu na kwamba hajawahi kukutana naye.

Tanzania Daima  pia lilinasa mawasiliano ya kutumiana fedha kutoka kwa Kapuya kwenda kwa binti huyo.

Baadhi ya mawasiliano hayo ni pamoja na yale yaliyofanyika Agosti 31 mwaka huu kupitia simu ya Kapuya ambapo alituma sh 300,000 kwenda kwa binti huyo kama sehemu ya makubaliano ya kutuma pesa kila mwezi kwa ajili ya matunzo.

Mawasiliano hayo ni kama ifuatavyo: U26UG365 Imethibitishwa Umepokea Tsh 300,000 kutoka kwa JUMA KAPUYA Tarehe 31/8/13 saa 3:28 PM Salio lako la M-PESA ni Tsh 300,000

V04EU470 Imethibitishwa Umepokea Tsh 400,000 kutoka kwa JUMA KAPUYA Tarehe 24/9/13 saa 2:38 PM Salio lako la M-PESA ni Tsh 400,040.

R93NY448 Imethibitishwa Umepokea Tsh 505,000 kutoka kwa JUMA KAPUYA Tarehe 21/6/13 saa 11:07 AM Salio lako la M-PESA ni Tsh 505,000.

Kutokana na mfululizo wa habari hiyo, Profesa Kapuya kupitia kwa wakili wake Yasin Memba, ametishia kuliburuza mahakamani Tanzania Daima endapo halitamwomba msamaha ndani ya siku saba.

Source: Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

Search This Blog